NMB ‘Masta Bata Kotekote’ msimu wa nne, Zaidi ya milioni 300 kutolewa

General / 11th November, 2022

Na Taji Silasi


Benki ya NMB imezindua msimu wa nne wa Masta Bata kotekote wenye lengo la kuwahamasisha wateja wake kutumia kadi kufanya malipo.


Hayo yamesemwa leo Nov 11, 2022 na Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam Donatus Richard wakati akichezesha droo ya kwanza ya Masta Bata Kotekote msimu wa nne ambapo mshindi wa mwanzo amepewa bodaboda huku washindi wengine 75 wakipewa fedha taslim shilingi 100,000.


Aidha Richard amesema droo hiyo itatolewa kila wiki ambapo mshindi atapata fedha taslim na wengine kushinda bodaboda, huku akiongeza kuwa droo hiyo kwa mwezi mshindi atapata bodaboda mbili na fedha taslimu kutolewa kwa washindi wengine. Grand finale washidni saba watapata fursa ya kwenda Dubai na Zanzibar ambapo kila mshindi ataweza kwenda na mwenzake au rafiki katika safari biyo.


Amesema Benki ya NMB imekuwa ikiendelea kuwahamasisha watanzania kupitia kampeni mbalimbali kutumia Zaidi kadi kufanya malipo badala ya mutumia fedha taslim ambapo pia kadi hiyo hutumika kufanya malipo ndani na nje ya nchi.


“Mnafahamu kwa muda mrefu tumekuwa na kampeni mbalimbali za kuhakikisha watanzania wanatumia Zaidi kadi na tumekuwa tukishirikiana na wenzetu wa Master card kuhakikisha tunaendeleza utamaduni huu wa kuitumia kadi  badala ya pesa taslimu.”


“Ukiwa na kadi yako unaweza kuitumia popote ukwia ndani au ukienda nje ya nchi.” Ameongeza Richard.


Katika hatua nyingine ametoa wito kwa watanzania kuendelea kutumia master card kufanya malipo ili kujiweka katika nafasi ya kushinda zawdi hizo za  Masta bata kotekote zilizoandaliwa msimu wa nne.


Naye Meneja Mwandamizi Idaraya Biashara za Kadi, Manfred Kayala amesema droo hiyo itachezeshwa kwa Zaidi ya miezi mitatu na kuwasisitiza wateja kuendelea kutumia zaidi kadi katika kufanya malipo.


“Wateja wetu mnashauriwa kutumia kadi badala ya kutumia pesa taslimu, ambayo tunajua kwamba pesa taslimu kutembea nazo inakuwa ni changamoto, zoezi hili tutakuwa tunalifanya kw takribani miezi Zaidi ya mitatu, na washindi nmbalimbali watapatikana”.