The Royal Tour Yatizamwa na Watu Bil 1.2

The Royal Tour Yatizamwa na Watu Bil 1.2

General / 30th April, 2023

Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii  na Mwenyekiti wa Kamati ya Rais ya Kuitangaza Tanzania, iliyoratibu maandalizi ya filamu ya Royal Tour, Dkt. Hassan Abbasi, amesema mwaka mmoja, tangu filamu hiyo izinduliwe hapa nchini, takribani watu bilioni 1.2 duniani, wameiona au kujihusisha na filamu hiyo kupitia taarifa za vyombo mbalimbali vya habari.


Dkt. Abbasi ameyasema hayo leo Aprili 28, 2023 alipokutana na wanahabari jijini Dodoma ikiwa ni mwaka mmoja tangu Rais Samia Suluhu Hassan alipoizindua filamu hiyo jijini Arusha mwaka jana.


“Mwaka mmoja leo Royal Tour imeleta mafanikio makubwa sana ikiwemo kuongeza watalii nchini maradufu, mapato ya utalii kuongezeka maradufu na hata mashirika mbalimbali ya ndege ya kimataifa kuongeza miruko ya kuja nchini,” alisema Dkt. Hassan Abbasi



Samia launches 'The Royal Tour' at United States promotion gala


Aidha, kumekuwa na ongezeko la mapato ya utalii maradufu ambapo mapato ya jumla ya sekta yameongezeka kutoka Dola za Marekani bilioni 1.310.34 sawa na Sh trilioni 3.01 mwaka 2021 hadi Dola za Marekani bilioni 2.527.77 sawa la Sh trilioni 5.82. Filamu hiyo ni maono ya Rais Samia Suluhu Hassan.


“Mwaka mmoja uliopita tulizindua Royal Tour na Watanzania waliiona rasmi, wakati tunatangaza Royal Tour hatukudhani kama tungefikia hapa,” alisema na kuongeza kuwa taasisi zote kubwa duniani zilizoifanyia ulinganifu na alama Filamu ya Royal Tour zimeipa alama kubwa pengine kuliko Royal Tour nyingine nane.


Alisema kuwa Mtandao wa TripAdvisor: Mtandao namba moja duniani katika kutangaza utalii umeipa Royal tour alama 5/5; Mtandao wa Amazon Video; umetoa alama 4.5/5; na Mtandao wa IMDb; Mtandao namba tatu duniani baada ya Youtube na Netflix umeipa Royal Tour alama 8.8/10.


Alisema kuwa kwa mujibu wa ripoti ya waandaaji wa Royal Tour, filamu hiyo si tu imeshaoneshwa katika vituo zaidi ya 300 vya televisheni vilivyoko kwenye majimbo yote Marekani, lakini tofauti na Royal Tour nyingine zote, filamu ya Tanzania imetajwa kuwa namba moja kwa kutazamwa zaidi na vituo vingi vya televisheni kulazimika kuirudia na vinaendelea kuirudia.


“Kwa mujibu wa ripoti ya Kampuni ya Peter Greenberg Worldwide (PGW), kawaida kiwango cha kutazamwa filamu za Royal Tour katika majimbo inakooneshwa hufikia wastani wa asilimia 67, lakini Royal Tour ya Tanzania imefikisha wastani wa kihistoria wa asilimia 81,” alisema



Alisema kuwa kupitia mafanikio haya Tanzania sasa imepata morali ya kwenda kimataifa zaidi kuitangaza Tanzania: Royal Tour sio mwisho ni mwanzo wa kuitangaza nchi kimataifa zaidi hivyo Kamati mwaka mmoja sasa, imepokea na inaendelea kuchambua “Royal Tours