Shilingi bilioni 185 kupanua shughuli za uzalishaji pamoja na kuleta fursa mpya za ajira
Naibu Waziri Wizara ya
Uwekezaji, Viwanda na Biashara Exaud Kigahe kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji,
Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji ametoa wito kwa Wakulima kutumia fursa
ya kuongeza uzalishaji wa malighafi.
Naibu Waziri Kigahe Ameyasema hayo Tarehe 22
Novemba, 2022 aliposhiriki hafla ya upanuzi wa kiwanda cha kutengeneza Vinywaji
vikali cha Serengeti Breweries Limited (SBL) kilichopo Mkoani Kilimanjaro.
Naibu Waziri Kigahe ameongeza kuwa Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatambua kwa dhati juhudi kubwa
zinazofanywa na Wawekezaji Nchini hasa katika kukuza uchumi na kufanya maisha
ya wananchi wetu kuzidi kuboreka hivyo kutokana na kiwanda kuongeza mstari wa
uzalishaji ni fursa kwa Wakulima kuongeza uzalishaji wa malighafi kwa ajili ya
kulisha kiwanda hiki.
Akizungumza kwa niaba ya Kampuni Mkurugenzi
Mwendeshaji wa Kiwanda cha Serengeti Breweries Mark Ocitti amesema, Kampuni
imewekeza kiasi cha Shilingi bilioni 185 katika kupanua shughuli za uzalishaji
ambapo italeta fursa mpya za ajira, kuongeza mapato ya serikali na kuwanufaisha
wadau wote wa Biashara hii.
Aidha, Ocitti ameongeza kuwa Nchi ya Tanzania ina
hali ya hewa nzuri kwa Kilimo, idadi kubwa ya watu na hivyo kuvutia Uwekezaji
katika Viwanda na Serikali ya awamu ya Sita imeboresha Mazingira ya Biashara
Nchini kwa Wawekezaji wakubwa na Wadogo na changamoto zilizokuwa zinajitokeza
zimekuwa zinasghughulikiwa kwa wakati.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mahusiano John
Wanyancha amesema Kiwanda cha Serengeti Breweries tawi la Moshi asilimia sabini
(70) ya malighafi inayotumika kiwandani hapo inatoka kwa wakulima wa ndani ya
Nchi, na kiwanda kimeongeza matanki kumi (10 ) ya kuchachulia pombe, mstari
mpya wa kupakia na sehemu ya uzalishaji wa pombe kali aina ya Sminorff Ice
nyekundu na Nyeusi.