NMB Yatoa msaada wa vifaa tiba Zaidi ya Mil. 26
Benki
ya NMB imetoa msaada wa vifaa tiba vyenye thamani ya Zaidi ya Shilingi Milioni
26 Wilaya ya Arusha katika kuunga mkono juhudi za Serikali kuboresha huduma za
Afya nchini.
Miongoni mwa msaada huo ni pamoja na vitanda 10 vya kujifungulia kwa kina mamana
Vitanda
10 vya kulazia wagonjwa wa kawaida.
Kabla
ya kukabidhi vifaa hivyo, Afisa Mkuu wa Huduma Shirikishi wa NMB, Nenyuata
Mejooli amesema kuwa vifaa hivyo ni moja ya ushiriki wetu katika maendeleo ya
jamii na wao kama benki inayoongoza Tanzania, wanao wajibu wa kuhakikisha jamii
inayowazunguka inafaidika kutokana na faida wanayoipata.
Aidha aliongezea kuwa Benki ya NMB imekuwa
ikipokea maombi mengi sana ya kuchangia katika miradi ya jamii, lakini benki
imejikita zaidi katika maeneo ya elimu, afya, na misaada ya hali na mali katika
nyakati ngumu kama za majanga na tumekuwa mstari wa mbele kuchangia huduma za
kijamii kwa lengo la kurejesha sehemu ya faida yetu kwa jamii.
kwa zaidi ya miaka kumi mfululizo, Benki ya NMB
imekuwa ikitenga asilimia 1℅ ya faida yake kama sehemu ya uwajibikaji kwa jamii
inayoizunguka.