Kampeni ya Umebima yazinduliwa Dar

Kampeni ya Umebima yazinduliwa Dar

General / 23rd February, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Hashim Komba (wa tatu kulia), akipeperusha bendera na Mkuu wa Idara ya Bima wa Benki ya NMB, Martine Massawe (wa tatu kushoto) kuashiria uzinduzi wa Kampeni ya Umebima kwa Kanda ya Dar es Salaam.
Uzinduzi huo umefanyika katika eneo la Stendi ya Simu 2000 jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Afisa Biashara Manispaa ya Ubungo, Geofrey Mbwana, Mkuu wa Idara ya Wateja Binafsi, Aikansia Muro (wa pili kushoto), Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Mbezi Louis, Ian Meena (kulia) na Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam, Donatus Richard (wa pili kulia).
Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam, Donatus Richard akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Umebima wilaya Ubungo.
Mkuu wa Idara ya Idara ya Bima ya NMB, Martin Massawe akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Umebima wilaya ya Ubungo.