BOT: Marufuku Kukopesha Bila Leseni
Benki Kuu ya Tanzania imebaini kuwa kuna baadhi ya taasisi,
kampuni na watu binafsi wanaojihusisha na biashara ya kutoa mikopo bila leseni,
Jambo ambalo ni kinyume na kifungu cha
16(1), cha sheria ya huduma ndogo ya fedha yam waka 2008.
Hivyo Benki Kuu inapendaa kuutaarifu umma kuwa, taasisi,
kampuni na mtu binafsi wasio na leseni husika hawaruhusiwi kufanya biashara ya
kukopesha.
Aidha kwa mujibu wa mujibu wa kifungu cha 16(2)(a) cha
sheria ya huduma ndogo ya fedha mwaka
2018, hatua zitakazochukuliwa kwa ukiukaji wa sheria hiyo, ni pamoja na faini
ya shilingi Milioni 20 au kifungo kisichopungua miaka miwili.
Hata hivyo Banki Kuu ya Tanzania imewaasa wananchi kuepuka
kufanya biashara na kukopa kwa taasisi, watu binafsi ambao hawana leseni.
Na orodha ya taasisi, kampuni na watu binafsi wenye leseni za biasshara ya kukopesha zilizotolewa na banki kuu ya Tanzania inapatikana kwenye tovuti ya banki kuu ambayo ni www.bot.go.tz.