BoT kuchukua hatua kudhibiti mfumuko wa bei nchini
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania
(BoT) Prof. Florence Luoga amesema kuwa kuimarika kwa Sekta ya Benki nchini
kunatokana na usimamizi mzuri wa Benki Kuu ambayo ndio muangalizi Mkuu wa Sekta
hiyo, ambayo imekuwa ikichangia kuifanya iweze kuchagiza katika ukuaji wa
uchumi.
Prof. Luoga ameyasema hayo
Novemba 22,2022 katika Chuo cha Benki Kuu Jijini Mwanza wakati wa mahojiano na
waandishi wa habari katika Mkutano wa siku mbili wa mawasilisho ya mada
mbalimbali ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya maafali ya kwanza ya Chuo hicho yanayotarajiwa
kufanyika Novemba 25, mwaka huu.
Amesema hatua hiyo imetokana na
uwepo wa waatalamu wa uendeeshaji katika Sekta hiyo ambao wamechangiza kueendelea
kuimarika kwa sekta ya benki ambayo imekuwa na mchango mkubwa katika ukuaji wa
uchumi wa Tanzania.
Prof. Luoga amesema kuwa Benki
hiyo imeendelea kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha mfumuko wa bei haukui na
kuleta athari za kiuchumi kwa Taifa.
Amesema kuwa mfumuko wa bei Tanzania bado ni mdogo
ambao ni asilimia 4.8 ikilinganishwa na nchi nyingine za Bara la Afrika na
Ulaya ambazo hivi sasa zinakaribia asilimia 10 na zaidi na kwamba Tanzania
imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kudhibiti mfumuko wa bei kutokana na wataamu wake
kufanyakazi kwa weledi kuhakikisha kunakuwepo na udhibiti wa viashiria
vitakavyosababisha kuwepo kwa athari hiyo.
“Kwa
Tanzania kuwa na mfumuko wa asilimia 4.8 hiyo sio bahati bali imetokana na
wataalamu wetu wanavyoweza kuangalia viashiria vya mfumuko wa bei kuongezeka
ghafla na kuchukua hatua ya kuhakikisha mfumuko wa bei hautokei kwa ghafla
hiyo. Kwa hiyo kuna hatua maalum ambazo sisi tunazichukuwa Ili kuilinda
nchi dhidi ya mfumuko wa bei” amesema Profesa Luoga.
Gavana wa Benki Kuu ya tanzania (BoT) Prof. Florence Luoga akizungumza alipokuwa katika Mkutano wa siku mbili wa mawasilisho ya mada mbalimbali ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya maafali ya kwanza ya Chuo hicho yanayotarajiwa kufanyika Novemba 25, mwaka huu.
katika hatua nyinge Prof. Luoga amezungumzia umuhimu
wa wataalamu wa Sekta ya fedha kuendelea kufanya utafiti ili kupata ufumbuzi wa
changamoto mbalimbali zinazoikabili Sekta hiyo ambapo amezungumzia umuhimu wa
uwepo wa Chuo cha Benki Kuu kilichojikita katika kuhakikisha kinazalisha
wataalamu watakaokwenda Kusimamia Sekta ya Benki.
“Chuo chetu kimejikita katika kuhakikisha Sekta ya mabenki inapata
wataalamu ambao watasimamia Sekta hiyo”
“Chuo
chetu Kwa kushirikiana na vyuo vingine nchini vinaweza kuelekeza nguvu na
juhudi za kufanya utafiti katika eneo zima la usimamizi wa Sekta ya fedha
nchini”
Hii
ni Sekta ambayo inasimamiwa na Benki Kuu na ndiye mshauri Mkuu wa Serikali,
ndio maana katika eneo zima la usimamizi wa Sekta ya fedha Benki Kuu lazima iwe
huru kwa kushirikiana na wataalamu ambao inawategemea kuhakikisha kuwa
utafiti unafanyika na ufumbuzi unapatikana kabla athari hazijatokeza. Ndicho
kitu tunachokifanya leo kuangalia tumefikia wapi katika kutayarisha wataalamu,
tumefikia wapi katika kufanya utafiti, kwa kushirikiaha na wataalamu kutoka katika
Taasisi nyingine kuhakikisha kuwa tunakuwa na uwezo katika kufanya utafiti
kupata ufumbuzi na kutekeleza” amesema Prof. Luoga.
Chuo cha Benki Kuu ya Tanzania kitafanya Maafali
yake ya kwanza Ijumaa Novemba 25, 2022 toka kuanzishwa kwake na kuwa na jumla
ya wahitimu 36 waliofanya vizuri na kufaulu masomo yao.