ATCL yaongeza idadi ya safari kwenda india na china

ATCL yaongeza idadi ya safari kwenda  india na china

General / 22nd February, 2023

Ili kupanua Wigo wa biashara nchini Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) limeongeza  safari zake za  nje ya Nchi  pamoja na kupunguza gharama za Usafiri wa ndege lengo likiwa ni kuwawezesha wafanyabiashara kufanya  biashara zao kwa urahisi .

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ndege (ATCL) Ladislaus Matindi wakati akizungumza na waandishi wa habari Leo Jijini Dar es Salaam, ambapo amesema Shirika limeamua kupanua mtandao wa safari kwa ndege zenye masafa ya mbali (Dream liner) zinazofanya  safari kutoka Tanzania kwenda India na nyingine kutoka Tanzania kwenda China.

Aidha Matindi amesema Kuongezeka kwa safari hizo pamoja na kupungua kwa gaharama  kwenda nje  ni kutokana   kupunguzwa kwa masharti ya UVICO_19 hivyo sasa safari za kwenda China zitakuwa mara mbili kwa wiki na kwenda India itakuwa mara nne kwa wiki.

Mbali na hayo Matindi amesema ili kuendelea kuboresha Shirika Hilo hivi karibuni Ndege mbili zinatarajiwa kufika nchini mwaka huu ambapo Ndege moja itaingia mwezi wa nane na mwisho wa mwaka huu

Katika hatua nyingine ametoa wito kwa wananchi kuchangamkia fursa  za Ajira zilizopo kwenye Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) kama vile uhasibu, uhudumu wa kwenye ndege, Urubani na nyingine nyingi ambazo zitatokea kupitia ujio wa ndege hizo mpya.

Ikumbukwe kuwa shirika la ndege Tanzania lilipunguza safari zake za nchi ya nje baada ya kuwepo kwa janga la ugonjwa wa COVID-19 lililoingia nchini 2020.