Wanawake wajawazito 200 wapatiwa msaada Vifaa wakati wa kujifungua.
Wanawake
wajawazito wameshauriwa kuzingatia lishe bora inayoambatana na kufanya mazoezi
mara kwa mara wakati wote wa ujauzito ili kulinda afya ya mama na mtoto
itakayosaidia kupunguza vifo vinavyotokana na uzazi.
Hayo
yamesemwa leo Novemba 18, 2022 na Theodora Malala akimwakilisha Mkuu wa Wilaya
ya Temeke Joketi Mwegelo katika uzinduzi wa mbio za Temeke Maternal Jogging
zenye lengo la kuihamasisha jamii kuhusiana na uhusiano uliopo kati ya lishe
bora wakati na baada ya ujauzito utakaosaidia kujenga kizazi bora.
Theodora
ameishukuru Taasisi ya Hatua Group Afrika kwa kuwapatia vifaa vinavyotumika
wakati wa kujifungua kwa kina mama wapatao 200 na kutoa wito kwa kina mama hao
kuzingatia lishe bora pamoja na kufanya mazoezi hata baada ya kujifungua.
“Tunawashukuru
sana na zawadi hizi tutaenda kuzitoa kwenu, tukiamini itakuwa ni kotisha ya
kuendelea kukumbuka kwamba tulifanya jambo hili Fulani, siku Fulani katika
hospitali ya Rangitatu ambayo itaturahisihia sisi tuwe tunakula vizuri, lakini
vilevile tuzingatie mazoezi na tuhudhurie kliniki”. Amesema Theodora.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa Hatua Group Afrika Derick Mgaya amesema taasisi hiyo ilianzisha programu
ya Busela ili kutoa elimu kwa wanawake wajawazito juu ya namna bora ya kupata
lishe bora, kuwahamasisha kufanya mazoezi pamoja na kuwapatia ushauri wa
saikolojia.
Ameongeza
kuwa mpaka sasa wamefanikiwa kuwafikia wanawake Zaidi ya elfu mbili huku lengo
likiwa ni kuwafikia wanawake laki tatu nchini ifikapo 2024.
Sabrina
Shabani ni miongoni mwa wanawake waliopata msaada huo ameishukuru Taasisi hiyo
kwa kutoa msaada kwa kina mama wajawazito pamoja na elimu waliyopatiwa kuhusu
umuhimu wa lishe bora.
Mbio hizo
za Temeke Martenal Jogging zenye kauli mbiu isemayo ‘Ujauzito wenye Afya, Utoto
wenye Afya’ zinatarajia kuanza Februari mwaka 2023.