Wakurugenzi wa Idara na Taasisi watakiwa kuongeza kasi kuhudumia wananchi
Naibu Waziri Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na
Biashara Exaud Kigahe Kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara
Dkt. Ashatu Kijaji amewataka Wakurugenzi wa Idara na Wakuu wa Taasisi zilizo
chini ya Wizara kuongeza kasi ya kuwahudumia Wananchi hasa wawekezaji wa ndani na
Nje ya Nchi kwani Wizara hio ndio mhimili wa uchumi wa Nchi hii.
Naibu Waziri Kigahe ameyasema hayo tarehe 9
Januari, 2023 katika ofisi ya Hazina ndogo Mkoani Morogoro alipofungua kikao
kazi cha Katibu Mkuu wa Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara na Wakuu wa
taasisi zilizo chini ya Wizara kwa lengo la kujadili mkakati madhubuti wa
utekelezaji wa majukumu na kubadilika kiutendaji ili kufikia adhma ya serikali
ya awamu ya sita ya kuifanya Tanzania kuwa chaguo la kwanza la wawekezaji ili
kuongeza ajira kwa watanzania kupitia sekta ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara.
Awali akimkaribisha Naibu Waziri, Katibu Mkuu
Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara Dkt. Hashil T. Abdallah ambaye ametoa
shukrani za pekee kwa Naibu Waziri kuwa sehemu ya kikao kazi hicho ambacho
kinaenda kuonesha dira na mwelekeo wa Wizara.
Dkt. Abdallah amesema kuwa lengo la kuwaleta
pamoja wakuu wote wa taasisi zilizo chini ya Wizara ni kujadiliana kwa pamoja
namna bora ya kutatua changamoto zinazowakabili wafanyabiashara nchini na kuja
na mkakati madhubuti wa kiutendaji ili kuendana na kasi ya Serikali ya awamu ya
sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu
Hassan.
Kikao kazi cha Katibu Mkuu kimehudhuriwa pia na
Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji Bw. Ally Gugu, Wakurugenzi wa
Idara kutoka Wizara ya Uwkezaji, Viwanda na Biashara na Wakuu wa Tasisi zilizo
chini ya Wizara.