Serikali yasema iko tayari kufanya chochote kupunguza bei ya mafuta

General / 5th May, 2022

Waziri wa Nishati, January Makamba amesema Serikali iko tayari kufanya chochote ili kukabiliana na changamoto ya kupanda kwa bei za mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa nchini.

Akichangia hoja iliyotolewa na Mbunge wa Kilindi (CCM), Omary Kigua ya kupanda kwa bei ya mafuta leo Mei 5,2022, Makamba amesema jana Serikali ilikaa kutazama hatua za kuchukua za haraka za kukabiliana na changamoto hiyo.

Amesema hatua za kikodi zinataka mashauriano, ufuatiliaji wa sheria na kanuni zinaongoza uwekaji na uondoaji wa hizo tozo.

Amesema ushauri uliotolewa na wabunge wa kuondoa kodi wamelichukua lakini suala hilo linataka uzingatiaji wa sheria na kanuni zake na taratibu za nchi zinazohusiana na masuala ya kodi.