Rais Samia achangia Mil. 70 Kwa watoto Njiti
Rais Samia Suluhu Hassan
amechangia shilingi milioni 70 kwenye taasisi ya Doris Mollel Foundation,
ambapo shilingi milioni 20 ni kwa ajili ya kuwasaidia watoto Njiti kupitia
taasisi hiyo na vifaa tiba vya kuwasaidia watoto Njiti vyenye thamani ya
shilingi Milioni 50.
Mkurugenzi wa taasisi ya Doris Mollel Foundation,
Doris Mollel amemshukuru Rais Samia kwa msaada huo na kuongeza kuwa msaada huo
umetolewa katika wakati mwafaka.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin
Mollel amesema, fedha hizo ni za Rais mwenyewe kutoka kwenye mshahara wake na
amemshukuru kwa msaada huo.
Ameongeza kuwa serikali kupitia wizara ya Afya
itaendelea kuwasaidia watoto Njiti pamoja na wanawake wanaojifungua watoto
Njiti.
Taasisi ya Doris Mollel Foundation hapo jana
iliadhimisha Siku ya Mtoto Njiti Duniani, maadhimisho yaliyofanyika wilayani
Serengeti, mkoani Mara.
Maadhimisho ya Siku ya Mtoto Njiti Duniani
yalifanyika duniani kote tarehe 17 mwezi huu.