NIC Yatoa Gawio Kwa Serikali
Shirika la Bima la Taifa NIC limetoa gawio ya Sh.Bilioni 1.5 kwa Serikali baada ya kufanya vyema kwa miaka minne mfululizo na kuweza kupata faida ambayo imekwenda kutoa gawio hilo.
Shirika hilo kutokana na faida hiyo inakwenda kuongeza mitaji na shirika wa Bilioni 12.05 ambapo kunafanya NIC iweze kuwa na uwezo mkubwa ushindani katika soko .
Akizungumza na waandishi wa habari leo Aprili 20,2022 Jijini Dar es Salaam,Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa NIC, Laston Msongole amesema kwa kipindi cha miaka minne mfululizo iliyopita kwa hesabu zilizokaguliwa inayonyesha kufanya vizuri baada ya taarifa ya hesabu ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu Hesabu za Serikali (CAG).
Amesema shirika limeendelea kuwa imara kwa kuongeza faida ambapo shirika hilo halijawahi kutoa gawio kwa serikali kwa miaka 30 iliyopita.
“Miaka minne mfululizo iliyopita kufikia mpaka Juni, 2021 ambapo tunahesabu zilizokaguliwa, Shirika limekuwa na maendeleo yakutosha na hilo linathibitishwa na taarifa CAG ampapo kila mwaka anakagua”. Amesema
Amesema katika kipindi cha mwaka 2018, Shirika lilipata faida ya bilioni 3.63, mwaka uliofuatia ambao ni 2019 likapata bilioni 7.79, mwaka 2020 likapata bilioni 33.65 na mwaka unaoishia Juni,2022 wamepata bilioni 73.10 hivyo Shirika limeendelea kuongeza faida kila kukicha.
Aidha Msongole amesema kuwa matarajio yao kufikia mwakani kwa maana hesabu za kukaguliwa kufikia Juni 2022 hesabu hiyo itakuwa mbali na hiyo ambayo wamefikia kwa sasa.
Pamoja na hayo amesema kwa mafanikio hayo waliyoyapata wanatarajia kutoa gawio kwa Serikali kutokana na mafanikio makubwa ambayo yamepatikana kwa miaka minne kwa kuongeza mtaji.
Kwa upande wake Msajili wa Hazina Mgonya Benedicto amesema Shirika hilo limejiweka vizuri katika kudhibiti matumizi yasiyo na tija na kwa wakati huohuo limeendelea kujenga imani kwa watanzania ambapo hivi sasa ni idadi kubwa kwa wanaokata bima kwenye shirika hilo.
Ameeleza kuwa katika majadiliano yao kupitia mahesabu ya shirika, ile faida ambayo imepatikana sehemu wameamua kuimarisha mtaji wa shirika ambapo sasa utaiwezesha kufanya bioiashara kisheria ukilinganisha na hapo awali vilevile wamekubaliana shemu nyingine ipelekwe kwenye mfuko wa serikali kama gawio kwa serikali.
Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Dk. Elirehema Doriye amesema moja wapo ya mipango ambayo wamekuwa nayo kwa sasa ni katika uharaka wa utoaji huduma za Bima, kwasasa NIC linatoa huduma za Bima kwa maana ya ulipaji wa madai kwa muda mfupi kuliko shirika au kampuni yoyote Tanzania, ndani ya siku tano za kazi unapata malipo yako.
Amesema fedha hiyo inakwenda kwenda kuimarisha huduma ili kwenda kwa kasi zaidi na watu wataopata huduma kuwa sehemu ya mabalozi kutokana na ubora wa huduma zilizo NIC.
Amesema kwa mafanikio hayo yanatokana na wafanyakazi kufanya kazi kwa kujitoa vipawa vyao ikiwemo ubunifu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Taifa la Bima (NIC) Dk.Elirehema Doriye akizungumza mafanikio ya Shirika hilo kuhusiana na kutoa gawio kwa Serikali pamoja na kujiimarisha katika kutoa huduma bora za bima nchini,jijini Dar es Salaam.