Benki ya NMB yaibuka kinara tuzo za TRA

Benki ya NMB yaibuka kinara tuzo za TRA

General / 19th November, 2022

Benki ya NMB imeibuka kinara katika tuzo za mlipa kodi mkubwa zinazotolewa na Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA).

Benki hiyo imeshinda tuzo tatu zinazoitambua kama mlipa Kodi Mkubwa nchini kwa mwaka 2021/2022.


Tuzo hizo ni:

1️⃣ Mshindi wa Kwanza; Taasisi inayozingatia misingi na kanuni bora za ulipaji kodi.

2️⃣ Mshindi wa Kwanza; Mlipa kodi mkubwa zaidi katika kundi la taasisi za fedha nchini.

3️⃣ Mshindi wa Tatu; Taasisi inayolipa kodi kubwa zaidi nchini (sekta zote).


Mafanikio haya ni matokeo ya benki hiyo kuzingatia kanuni bora za ulipaji kodi, ufanisi katika kujiendesha na ubunifu wa suluhishi bora za kifedha zenye manufaa kwa wateja.

Benki ya NMB imedhamiria kuendelea kuendesha biashara yake kwa kuzingatia sheria na kanuni za nchi ili kuchangia kikamilifu ujenzi wa uchumi wa Taifa


WhatsApp%20Image%202022-11-18%20at%2012.52.02%20PM

Afisa Mtendaji Mkuu - NMB, Bi. Ruth Zaipuna akipokea moja ya tuzo kutoka kwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia, Mhe. Nape Nnauye wakati wa hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Wengine ni Afisa Mkuu wa Fedha - NMB, Bw. Juma Kimori(wa tatu kulia) , Meneja wa Uwajibikaji kwa Jamii - NMB, Bi. Lilian Kisamba pamoja na Meneja wa Kodi - NMB, Bi. Janeth Buretta.
DSC01540
DSC01635

DSC01664

DSC01769